Marriage Supper of the Lamb (Swahili version)

Karamu Ya Arusi Ya Mwana Kondoo Na Matukio Ya Enzi Za Mwisho Von:
Marriage Supper of the Lamb (Swahili version)

Language: Swahili, Lugha: Kiswahili

Kitabu hiki kina maneno ya unabii kutoka kwa Yesu KUHUSU HIVI KARIBUNI UNYAKUO. Baadhi ya vichwa SURA katika kitabu hiki:

Unyenyekevu, msamaha, kuishi katika dunia, lakini si kuwa "Kati ya Dunia", Rapture na karamu ya arusi ya Mwanakondoo, kujiandaa kwa ajili ya Unyakuo, Tamaa Kwa Dunia, Viongozi Je, huwezi kunifuata, kufanya maandalizi, Acha kupambana na kila mengine, mimi si kuchukua wewe kama una asiyetubu dhambi, milele yako ni Mizani, wachache sana wananiabudu Mimi, wala Tubuni kwangu, mimi Wanataka nafasi ya kwanza Au No Place, kuna dhiki kuu ijayo, wengi ambao wanadhani wenyewe tayari wanajidanganya wenyewe, una thamani kidogo wakati iliyobaki.

Maneno ya unabii kutoka kwa Yesu kuhusu ndoa Karamu ya Mwana Kondoo:

Kutakuwa na vitu vingi vyema sana mbele kwa wanangu watakaonyakuliwa. Acheni niwaonyeshe kidogo tu vile itavyokuwa: Wanangu watakapofika, watalakiwa na wapendwa wao: familia na marafiki wale tayari wako mbinguni. Nitakuwa nikiwatazama. Huu utakuwa wakati wa utukufu mkuu. Ni tunu ilioje kuungana na familia ulioikosa muda mrefu! Kisha wanangu watapelekwa hadi kwenye karamu ya arusi ya Mwana Kondoo. Nitawaongoza kwenye karamu hii.

Meza itaandaliwa kwa vitu tele. Vikorokoro vyote vitakuwako. Kila jambo kuhusu karamu hii litakuwa la kuwastaajabisha. Wanangu watakaa katika sehemu iliyoandaliwa kila mmoja wao na majina yao yatakuwa yameandikwa kwenye sehemu hiyo kwa dhahabu. Vyombo vyote vitakuwa vya dhahabu vilivyopambwa na vito. Kitambaa cha mezani kutakuwa cha hariri, na nyuzi za dhahabu. Nuru itang’aa na vikombe vyote vitakuwa vya dhahabu vilivyolainishwa na vito ukingoni.

Kutakuwa na zawadi kwa kila mmoja pahali watakapoketi. Zawadi hii itakuwa ni kumbusho la uhusiano wangu na huyo mwanangu. Kila zawadi itatofautiana na nyingine. Kila zawadi itakuwa na maana yake kwa kila mwana kuonyesa uhusiano wangu naye. Kutakuwa na vitu vingi vya kustaajabisha siku hiyo – siku ya karamu ya arusi yangu.

 

http://www.mediafire.com/download/b6a7bof593h9d9g/karamu-ya-arusi-ya-mwana-kondoo.pdf

 

http://www.smashwords.com/books/view/393554

 

http://sites.radiantwebtools.com/?i=15948

 

http://marriagesupper.wix.com/endtimescatalog

 

NOTISI: Unaruhusiwa kusambaza nakala za nyaraka hizi kwa njia zo zote zile. Iwe kwenye mtandao au chapa. Waweza kazisambaza nyaraka hizi zote au sehemu kadha. Tunakuomba unapozisambaza, uiweke notisi hii ndipo wengine waweze kujua kwamba wana ruhusa ya kuzisambaza. Kitabu hiki kinapatikana pia kama MP3 ama e-book kwenye tovuti: http//endtimes-prophecy.com


Beiträge und Kommentare
Um eine optimale Funktionsweise zu gewährleisten, verwendet unsere Website Cookies. Durch die Nutzung der Website stimmst Du der Verwendung von Cookies zu. Mehr Infos
OK
Top of page
Kein Miniaturbild Entfernen Bitte wähle einen Grund aus Bitte gib die Stelle im Buch an. de de_DE